• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa Maranyingi |
    • Barua pepe za Watumishi |
Uyui  District Council
Uyui  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Kimsingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Administration and Human Resource
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Envinment and Sanitation
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za baraza la madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Mwekekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba Mbalimbali

VIKUNDI 14 VYA UYUI VYAKOPESHWA MILIONI 102.5

Imewekwa: December 15th, 2020

Vikundi 14 vya Wajasiriamali katika Halmashauri ya Wilaya ya Uyui vimepatiwa mikopo yenye thamani ya shilingi milioni 102.5 ikiwa ni sehemu ya asilimia 10 ya mapato ya ndani.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji Hemed Magaro wakati wa sherehe fupi ya kukabidhi mikopo hiyo kwa vikundi hivyo.

Alisema kati ya vikundi hivyo 9 ni vya wanawake ambavyo vimekopeshwa kiasi cha shilingi milioni 65 na vikundi 5 vya vijana vimekopeshwa shilingi milioni 37.5.

Magaro alisema hadi hivi sasa katika kipindi cha mwaka huu wa fedha wameshatoa kiasi cha shilingi milioni 85.6 ambayo ni sawa na asilimia 42 ya kiasi cha shilingi milioni 202.7 ambazo zinatakiwa kukopesha kwa vikundi vya walemavu, vijana na wanawake.

Mkurugenzi Mtendaji huyo alisema kuna madeni ya jumla ya shilingi 170.9 zinadaiwa kwa wakopaji ambapo kati ya hizo vikundi vya wanawake vinadaiwa shilingi milioni 58.4, vijana wanadaiwa shilingi milioni 96.2 na watu wenye ulemavu wanadaiwa milioni 16.2.

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Philemon Sengati aliitaka Halmashauri hiyo kuanza utoaji wa mikopo ya fedha nyingi na vifaa na zana mbalimbali ambazo zitawasaidia wananchi kuanzisha viwanda vidogo.

“Ifikie kipindi muanze kutoa mashine ili wananchi waweze kuwa na miradi mikubwa ambayo itaharakisha maendeleo” alisema

Alisema hatua hiyo itawasaidia kuwepo na matokeo makubwa katika maisha ya wananchi kutokana na aina ya mikopo waliyokopeshwa.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa aliwataka wakopeshaji kurejesha mikopo ili iweze kuwasaidia wengine kwa ajili ya kujikwamua kiuchumi na kujiletea maendeleo.

Mwisho

MAELEZO YA PICHA

   Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Philemon Sengati (katikati) akikabidhi mfano wa hundi ya shilingi milioni 102.5 kwa ajili ya mikopo kwa vikundi 14 ikiwa ni asilimia 10 inayotokana na mapato ya ndani.

Matangazo

  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021 December 19, 2020
  • Soma zote

Habari Mpya

  • MADIWANI UYUI WAPITISHA BAJETI YA SHILINGI BILIONI 34.2 MWAKA UJAO WA FEDHA

    February 16, 2021
  • MKUU WA WILAYA AKAGUA MIRADI YA UJENZI WA MADARASA HALAMASHAURI YA WILAYA UYUI

    January 06, 2021
  • VIKUNDI 14 VYA UYUI VYAKOPESHWA MILIONI 102.5

    December 15, 2020
  • TANGAZO LA UWEKAJI WAZI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA KUANZIA TAREHE 17/06/2020 HADI TAREHE 20/06/2020

    June 14, 2020
  • Soma zote

Video

SAMIA SULUH
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari Mpya

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Tabora RAS
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani
  • Watumishi Portal
  • Tabora MC

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Uyui District Council

    Anuani ya Posta: S.L.P 610

    Simu ya Mezani: +255 26 296 6008

    Simu ya Mkononi: +255 766616985

    Barua pepe: ded@uyuidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa Maranyingi
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2016 UyuiDC . All rights reserved.