• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali Yanayoulizwa Maranyingi |
    • Barua pepe za Watumishi |
Uyui  District Council
Uyui  District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Kimsingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Halmashauri
    • Idara na Vitengo
      • Administration and Human Resource
      • Planning,Statistics and Monitoring
      • Fedha na Biashara
      • Afya
      • Maendeleo ya Jamii
      • Elimu Sekondary
      • Elimu Msingi
      • Ujenzi
      • Maji
      • Envinment and Sanitation
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Ugavi
      • Ufugaji Nyuki
      • Uchaguzi
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
  • Huduma
    • Huduma za Afya
    • Elimu
    • Huduma za Maji
  • Madiwani
    • Orodha ya Waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu za baraza la madiwani
    • Ratiba
      • Ratiba ya Vikao
      • Ratiba ya Mwekekiti wa Halmashauri
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi Inayotekelezwa
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria Ndogo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa Umma
    • Hotuba Mbalimbali

KAMATI YA UJENZI YA SEKONDARI YA IDETE ILIYOPO WILAYANI UYUI YAPONGEZWA NA MWENGE WA UHURU

Imewekwa: July 18th, 2021

NA TIGANYA VINCENT,

Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Idete iliyopo Wilayani Uyui  John Paul Mdaki na Kamati yake ya Ujenzi imepongezwa na Viongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru kwa matumizi mazuri ya shilingi milioni 40 yaliweza kujenga na kukamilisha madarasa mawili.

Pongezi hizo zimetolewa leo na Kiongozi wa Mbio maalum za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi kwa niaba ya wenzake baada ya kukagua mradi huo na kuridhishwa na viwango vya ujenzi.

Amesema Mwalimu huyo na Kamati yake wameonyesha uzalendo mkubwa kwa kuweza kutumia milioni 36 kujenga madarasa mawili na kuweka samani kwa ajili ya matumizi ya wanafunzi 80 na walimu wawili wakati wa vipindi.

Luteni Josephine ameongeza kuwa Mwenge wa Uhuru sio tu unakosoa pia unasifia pale Watendaji wamapofanya vizuri kwenye miradi  ya umma na kuwataka watumishi wengine kuiga mfano wa Kamati ya Ujenzi ya shule ya Sekondari Idete,

“Mkuu wa Wilaya unaonaje kazi hii na Mwalimu Mkuu alivyo kwa kweli huyo anastahili  kupandishwa na kuwa Afisa Elimu kwa kazi yake nzuri”amesisitiza,

Awali Afisa Elimu Sekondari , Ndg Jacob Makala amesema kuwa hadi kukamilika kwa kazi zote wametumia jumla ya Shilingi milioni 36.9 na kubaki na kiasi cha milioni 3.

Katika hatua nyingine Mwenge wa Uhuru umetembelea na kuweka Msingi jumla ya miradi sita yenye thamani ya shilingi bilioni 2.7.

Wakati huo huo Kiongozi wa Mbio Maalum za Mwenge wa Uhuru Luteni Josephine Mwambashi ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Uyui kuhakikisha wanapeleka maji safi na salama yaliyopo katika mtandao wa Ziwa Victoria katika Josho la  Kijiji cha Kinyamwe ili wafugaji wawe na uhakika wa maji kwa ajili ya Josho lao.

Amesema mtandao wa maji ya ziwa Victoria uko karibu sana na Josho lao ni vema wakapelekewa maji hayo na kuachana na maji ambayo hayana uhakika,

Mkuu wa Wilaya ya Uyui Kisare Makori amesema kati ya fedha hizo Serikali Kuu  ni shilingi bilioni 2.2, Halmashauri ni milioni 223.6, michango ya wananchi milioni 297.3 na wadau wa maendeleo ni milioni 25.

Amesema mradi wa kwanza unahusu ufugaji wa nyuki katika Msitu wa Hifadhi wa Simbo ambao umegharimu milioni 58.2 na unaosimamiwa na Chuo cha Mafunzo ya Ufugaji Nyuki cha Tabora.

Makori ametaja mradi mwingine uliotembelewa na Mwenge wa Uhuru ni ule wa shughuli za uogeshaji wa mifugo kwenye Josho la Kijiji cha Kinyamwe ambao umegharimu milioni 898.

Ameongeza kuwa mradi mwingine ni ule wa uwekezaji wa sekta binafsi katika ujenzi wa majengo ya biashara katika eneo la Isikizya ambao hadi kukamika utagharimu milioni 290.

Makori amesema Mwenge wa Uhuru umetembelea Hospitali ya Wilaya ya Uyui kwa ajili ya kuangalia maendeleo ya ujenzi na ujenzi wa mfumo wa ukusanyaji taarifa za utoaji wa huduma za afya ambapo kazi zote zimegharmu bilioni 2.3 hadi hivi sasa.

Amesema Mwenge wa Uhuru pia umetoa zawadi kwa Msindi wa Kwanza hadi wa Tatu wa mashindano wa mpira wa miguu kwa wanaume ya Jimbo la Igalula ambayo yamegharimu milioni 25.

Mwisho

Maelezo katika Picha.


Kiongozi wa Mbio Maalumu za Mwenge wa uhuru Luteni Josephine Mwambashi akiweka Jiwe la Msingi leo uzinduzi wa Madarasa ya Sekondari ya Idete iliyopo Wilyani Uyui

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI September 09, 2021
  • TANGAZO LA KUPANGISHA MAENEO YA KUJENGA VIBANDA VYA BIASHARA STENDI YA MAGARI ISIKIZYA June 11, 2021
  • MAAGIZO YA KUJIUNGA NA MASOMO YA KIDATO CHA TANO KATIKA SHULE YA SEKONDARI IDETE June 08, 2021
  • TANGAZO LA KAZI YA KUCHANJA MIFUGO May 19, 2021
  • Soma zote

Habari Mpya

  • HALMASHAURI YA WILAYA UYUI YATOA MIKOPO YA SH.215,500,000 KWA WANAWAKE , VIJANA NA WENYE ULEMAVU

    January 13, 2022
  • MAHADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU WILAYANI UYUI

    December 09, 2021
  • HALMASHAURI YA WILAYA YA UYUI YATUMA BARUA YA PONGEZI KWA RAIS SAMIA

    November 02, 2021
  • KAMATI YA UJENZI YA SEKONDARI YA IDETE ILIYOPO WILAYANI UYUI YAPONGEZWA NA MWENGE WA UHURU

    July 18, 2021
  • Soma zote

Video

SAMIA SULUH
Video Nyinginezo

Viunganishi vya Haraka

  • Zabuni
  • Matukio
  • Matangazo
  • Habari Mpya

Tovuti Muhimu

  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Tabora RAS
  • Tovuti ya Baraza la Mitihani
  • Watumishi Portal
  • Tabora MC

World visitors tracker

world map hits counter

Waliotembelea

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Uyui District Council

    Anuani ya Posta: S.L.P 610

    Simu ya Mezani: +255 26 296 6008

    Simu ya Mkononi: (1) +255 766616985

    Barua pepe: ded@uyuidc.go.tz

Mawasiliano Zaidi

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali Yanayoulizwa Maranyingi
    • Ramani ya Eneo
    • Huduma

Copyright ©2016 UyuiDC . All rights reserved.